1. Suleiman aliamka asubuhi, akafanya nini?
2. Ni nani alimtoa kondoo
kibandani?
3. Kwa nini Hassan
alirudi bila kuchukuamzigo?
4. Kwa nini baba watoto
alikataa visu?
5. Kwa nini baba watoto
alimchuna kondoo kwa haraka?
6. Kwa nini ilikuwa
rahisi kumchuna kondoo wakati huo?
7. Suleiman alifanya nini
na matumbo?
8. Baba yake Suleiman
alimwambia Suleiman amletee nini pamoja na maji?
9. Ni nani walifagia
nje?
10. Wageni hawatapenda
kula nini?
Sarufi
A.
Tunga maneno ya kila kundi yawe sentensi.
Kwa mfano: mlinzi, wevi,
kuona, mlangoni, huyo, jana yatungwe kuwa
--> Jana, mlinzi huyo
aliwaona wevi mlangoni.
1. kesho, tatu, eropleni,kuruka, kutoka,
mpaka, Nairobi, Dar-es-Salaam
2. mwaka, katika,
1963, wa,kupata, Kenya, uhuru, wake
3. juzi, huyo,
kupanda,mkulima, mbegu, shambani
4. sasa, hivi,
kuandika,mwalimu, ubaoni, chaki, kwa
5. shingo, ni,
twiga, la, refu,shingo, kuliko, la, ng’ombe
B. Geuza sentensi
zifuatazo zionyeshe kuwa kitendo kimempata mtu anayetajwa katika alama kama
hizi:
Kwa mfano: Tajiri yule alimpa rafiki yake pesa nyingi. (mimi)
igeuzwe kuwa:
--> Tajiri yule alinipa pesa nyingi.
1. Mtoto
alimletea baba yake gazeti. (wewe)
2. Msafiri
alimwambia rafiki yake habari za nchi mbalimbali. (mimi)
3. Mwalimu atiwapa
wanafunzi vitabu vya Kiswahili. (sisi)
4. Wafanyi kazi
walimsaidia mtu kujenga nyumba kubwa. (ninyi)
5. Daktari mkuu
alimpa mgonjwa dawa nzuri. (wewe)
6. Gari
lilimharibikia Dillon njiani. (Amyna Angelique)