Home  |  Search  |  Help  |  Contact Us  |  Rutgers University Swahili


Practice
101 Assignments
101 Exercises
102 Assignments
102 Exercises
201 Exercises
202 Exercises
Discussion
“MSIBA WA KUJITAKIA”  

Wahusika

Mtoa muhtasari         mtu anayetoa muhtasari wa mtiririko wa vitendo pamoja na maelezo ya wahusika ndio nani na nani; habari hizi zatolewa kwa Kiingereza [Bi Maswali]

Mzee Mkali               mume mzee wa Mama Furaha; hataki mchezo  [Mwalimu]

Mama Furaha            mke kijana wa Mzee Mkali; apenda kutembea nje na vijana wa kiume wa rika lake  [Bi Mjuaji]

Furaha                        binti wa Mzee Mkali na Mama Furaha  [Bi Betty]

Sitaki                          kijana mpole  [Bw Shil]

Wabeya wawili     wanawake wa kawaida wanaokaakaa mitaani [Bi Nancy na Bi Megan]

Saada                          mchumbake Sitaki  [Bi Carol]

Msomaji wa barua     mtu asomaye barua ya kimapenzi ya Mama Furaha [Bi Jane]

Mfasiri wa barua        mtu anayefasiri kwa Kiingereza ile barua ya kimapenzi ya Mama Furaha [Bi Maswali]

-------------------------------------------------------------------

Mtoa muthasari:        Hamjambo nyote. On behalf of the students of Kiswahili at Rutgers University, I would like to extend a hearty welcome to each and everyone of you. I thank you for coming and I feel quite confident that you will enjoy our short play entitled “Msiba wa Kujitakia.” The word “msiba” in Kiswahili means a misfortune, a calamity, a tragedy, or some infelicitious circumstance. The title, “Msiba wa Kujitakia,” hence means a self-induced tragedy. The title is in reality an abbreviation of a Kiswahili proverb that says “Msiba wa kujitakia hauna kilio” which means roughly that one shouldn’t expect sympathy and understanding for trouble that he or she has caused by his or her own actions.

            This play, which was written jointly by the students in second and third year Kiswahili, has seven characters. They are:

Mzee Mkali, an elderly man with a very young wife;

Mama Furaha, the young and very flirtatious wife of Mzee Mkali;

Furaha, the teenage and quite urbanized daughter of Mzee Mkali and Mama Furaha;

Sitaki, a young man who is polite and somewhat shy;

Saada, the fiancée of Sitaki;

Two busybody women, who spend a large part of each day gossiping among themselves. 

            The first scene opens in the home of Mzee Mkali with him telling his wife that he’s going to town and that he might be late in returning. He also informs her that a young acquaintance named Sitaki will be dropping by and that she should tell him not to wait, that they will meet another day.     

Onyesha la Kwanza

Onyesho hili linaanza na Mama Furaha, mkewe Mzee Mkali, anashughulika na usafi nyumbani kwao. Baada ya kupita nukta 15 hadi 20 hivi, anaingia Mzee Mkali.  

Mzee Mkali:              Mama Furaha!

Mama Furaha:           Abee. 

Mzee Mkali:              Mimi natoka kidogo, naenda mjini. Nina shughuli moja muhimu. Siwezi kujua kwa hakika lakini huenda ikawa nitachelewa kurudi.

Mama Furaha:           Haya mume wangu. Nenda salama urudi salama.

Mzee Mkali:              Haya, nitajaribu kuharakisha mambo lakini unajua mambo yalivyo mjini siku hizi na ahadi za uwongo.

                                    Oh, nilitaka kusahau --- atakuja yule kijana Sitaki kuonana nami. Mwambie samahani, nitaonana naye siku nyingine.

Mama Furaha:           [akitabasamu na kuonyesha kufurahi sana] Sawa mume wangu.

                                     Mzee Mkali anageuka na kuondoka.

  [PAZIA]

Mtoa muthasari:        Scene two opens with Mama Furaha making herself attractive in hopes of attracting the attention of the young man who will be stopping by to see Mzee Mkali, who as we know, has gone to town. Mama Furaha’s young and impulsive teenage daughter tells her that she is going to the movie with a young male friend and this upsets Mama Furaha. The daughter makes a fast exit when the young man, Sitaki, arrives. The rest of scene is devoted to Mama Furaha and her attempts at seducing Sitaki. 

Onyesho la Pili 

Mzee akitoka Mama Furaha anaanza kujipambapamba. Ghafla binti yake anatokea. Anamwambia mamake anatoka. 

Furaha:                       Mama, mama, mimi naenda sinema. 

Mama Furaha:           Nini? Unaenda wapi? Sinema? Sasa hivi? Unaenda na nani?

Furaha:                       Na rafiki yangu. 

Mama Furaha:           Rafiki yako nani? Si yule mhuni Hamisi? 

Furaha:                       Mamaaa, yeye si …. 

Wakati huohuo sauti inasikika mlangoni ikibisha hodi. Furaha anaenda mlangoni na kuufungua.

Furaha:                       Ohh, karibu, karibu Bw Sitaki.

Akiingia Bw Sitaki, wakati uleule Furaha anatoka nje huku anakimbia. Anasikika kusema, “Kwa heri mama!”

Mama Furaha:           [akisema kwa sauti nyororo]  Karibu Ndugu Sitaki, karibu, karibu sana. 

Sitaki:                         Asante Mama Furaha.  Habari za hapa nyumbani?

Mama Furaha:           Salama kabisa. Mambo hapa nyumbani poa. Tuko wazima wote. Habari za utokako wewe? 

Sitaki:                         Sisi twamshukuru Mwenyezi, sote ni wazima wa afya.  

Mama Furaha:           Na mimi nimefurahi kusikia hayo.                     

                                    [Nukta 5 hivi zinapita katika hali ya ukimya.] 

Mama Furaha:           Karibu ukae kaka. 

Sitaki:                         [uso wake ukionyesha wasiwasi]  Mzee yupo? 

Mama Furaha:            Hayupo, katoka kidogo, ameenda mjini. Lakini amesema atarudi moja kwa moja. 

Sitaki:                         [akionyesha kusitasita kidogo] Ahh, labda niende.  

Mama Furaha:           Kaa bwana mdogo, usiende. Haki ya Mungu hatachelewa kurudi. Ataingia sasa hivi.   

                                    [Anamwonyesha kiti na kumwashiria akae. Sitaki, akionyesha wasiwasi, anakalia kiti polepole na taratibu.] 

Nikuletee nini? Kuna soda, kuna maji, kuna maji ya matunda, kuna chai, na kahawa. 

Sitaki:                         [akionyesha kufikiri kidogo.] Nadhani chai itanitosha. 

Mama Furaha:           Haya nakuja. 

                                    [Anageuka na kuondoka. Akiwa jikoni, kabla hajaanza kushughulika na utayarishaji wa chai ya mgeni, anaonekana akiandika harakaharaka maneno fulani kwenye karatasi. Kumaliza hayo, anakunjakunja karatasi hiyo na kuitia mfukoni mwake. 

                                    Baada ya dakika moja hivi kupita Mama Furaha anarudi huku akibeba sinia yenye kikombe, birika, kijiko, na sukari. Anaweka sinia juu ya kimeza na kukivuta kimeza hicho mbele ya Sitaki.]

                                   Karibu chai. Leo hakuna maziwa kwa hiyo ni chai ya rangi tu. Samahani. 

Sitaki:                         Bila samahani. Chai ya rangi inatosha kabisa. Ahsante Mama Furaha. 

Mama Furaha:           [akikaa kwenye kiti karibu na kijana Sitaki.] Ni muda mrefu hatujakuona. Mbona unatususa hivi? 

Sitaki:                         Siwasusi ila nilikuwa na kazi nyingi. 

                                    [Nukta mbili tatu za kimya zinapita. Sitaki anakunywa chai yake huku Mama Furaha anamkodolea macho … macho ya huba. Wasiwasi wa Sitaki wazidi kuongezeka. Mwishowe inambidi Sitaki kuuliza.] 

                                    Mama Furaha, una hakika Mzee atarudi sasa hivi? Hatachelewa mjini? 

Mama Furaha:           [Anamjibu huku anamkodolea macho ya “wasiwasi ondoa kijana mwenzangu, mimi ni wako” …] Amesema hatachelewa. Lakini hata akichelewa kidogo, naona si vibaya, siyo?  

                                    [Anasogeza kiti chake karibu naye na anaanza kumpapasapapasa mabegani huku akitamka hivi:]  Kwa kweli, mimi natumai atachelewa sana tupate kujuana vizuri zaidi au siyo kijana mwenzangu? 

Sitaki:                         [akionyesha kuogopa] Mimi nadhani bora niende sasa. Nitarudi baadaye akisharudi Mzee. 

                                    [Anaanza kuinuka toka kwenye kiti lakini Mama Furaha anamzuia huku anazidi kumpapasapasa na kumwambia maneno ya huba.] 

Mama Furaha:           Usiende mpenzi, nakupenda sana sana sana. Usiende mpenzi. Tafadhali nakuomba. Na ukienda, tuende wote.  

[PAZIA] 

Mtoa muthasari:        Scene three opens with two local female gossips outside the house of Mzee Mkali. They are talking, laughing, slapping five, and pointing towards the house. Suddenly Bi Saada, the fiancée of Sitaki appears. The two gossips tell her their suspicions. Saada seems at first not to believe them, but eventually she becomes pissed off. 

Onyesho la Tatu

Wabeya wawili nje ya nyumba ya Mzee Mkali wakipigana soga. Wanachekacheka na kugongana viganja. Mmojawao anaelekeza kidole kwenye nyumba: 

Mbeya wa 1:              Ahh, jamani, wanafanya nini humo ndani muda wote huu? 

Mbeya wa 2:              Na Mzee hayupo! Lakini si unajua tabia zake Mama Furaha? Basi, ole wao Mzee akiwafumania leo. Huyo mzee ni moto wa kuotea mbali, ni mtu wa hatari kwelikweli. Hana mchezo. 

Saada                          [Wakati huohuo anatokea Bi Saada, mchumbake Sitaki] Vipi shoga, unaongea juu ya nani? Kulikoni nyumbani kwa Mzee Mkali? 

                                    [Wote wanaangua vicheko]. .

Mbeya wa 1:              Bi Saada, nafikiri mali yako iko hatarini dada yangu. Yule mwizi wa mitaani Mama Furaha anajaribu kupindua kitanda chako. Mchumbako Sitaki yumo ndani, yuko naye, na Mzee Mkali hayupo. Wako peke yao. 

                                    Saada kwanza anaonyesha kutoamini lakini baadaye sura yake yabadilika na kuonyesha kaudhika sana. 

 

[PAZIA] 

Mtoa muhtasari:        This is the fourth and final scene. This is where Mama Furaha is caught red handed and her infidelity exposed. Happily, however, Sitaki and his fiancée, Bi Saada, are still in love and their relationship remains intact. Check it out. 

Onyesho la Nne                                   

Ghafula mlango unafunguliwa na anaingia Mzee Mkali kwa kishindo. Kimya kimya bila mtu kutambua, Saada naye aingia nyumbani kwa Mzee Mkali lakini anakaa pembeni pasi na kusema.  

Mzee Mkali:              [kwa sauti nzito na paazi]  Doo, masalale!!!  Ama, kunatukia nini humu? [akimgeukia Sitaki] Wee kijana unajaribu kuniibia “mali” yangu wakati mimi sipo? 

Sitaki:                         La, la, la … sio mimi Mzee, sio mimi! 

Mama Furaha:           [akiinuka haraka na kujifanya ameshikwa na woga] Ohh, mume wangu, Mungu mkubwa, kweli Mungu mkubwa. Nilikuwa nikiomba kuwa ungerudi kwa wakati maana huyu kijana amekuwa akinisumbua siku nyingi.  

Mzee Mkali:              [akianza kumsogelea Sitaki huku anamtemea vitisho] Wewe wafikiri mimi mtu wa kuchezewa? Hapana, leo utanitambua. Leo utanitambua na utajuta kuzaliwa. Hapana kwenda mahakamani. Leo kesi hii itasikilizwa hapahapa.  

[akimnyoyeshea kidole Sitaki] Mimi nitakukatakata vipande vipande hata mama yako itamwia vigumu kukutambua. 

Sitaki:                         Hapana Mzee. Mkeo anasema uwongo. Haikuwa mimi. Mimi sikumwanza mke wako, bali yeye ndiye aliyejaribu kunitongoza mimi. Wallahi Mzee, sikuongopei. Kweli sikuongopei. 

Mama Furaha:           Mwongo mkubwa huyu kijana . Usismsikilize na maneno yake ya uwongo. Yeye anajaribu kujisalimisha tu! Ni mwongo mkubwa. 

                                    Ghafula macho ya Mzee Mkali yananata kwenye kipande cha karatasi iliyokunjwakunjwa na iko sakafuni si mbali na miguu ya mzee huyo. Mzee anapoanza kuinama chini ili kuiokota karatasi ile, sura ya Mama Furaha  inabadilika na kuonyesha hofu kuu. 

Acha hiyo mume wangu … acha tu. Ni takataka. Nilikuwa nafagia nilipoingiliwa na huyu mhuni (ambaye si rafiki yako). Nipe mimi nitaitupa. 

Taratibu Mzee Mkali anaikunjua na kuisoma kwa sauti huku Mama Furaha anaonyesha kushikwa na woga akitafunatafuna kucha zake. 

Mzee Mkali:              [akisoma kimyakimya] 

Msemaje wa kike:     [akisoma kwa sauti barua hiyo] 

Mpenzi Sitaki,

                                                Mbona unaonyesha kutoelewa jinsi ninavyoingiwa na mahaba juu yako. Nakuota saa zote siku zote. Nimejaribu kukuonyesha dalili nyingi kisirisiri lakini wewe ama huzioni au hutaki kuziona. Mbona wanitesa bure mie kijana mwenzako?

                                                Nimechoka na maisha na Mzee Mkali. Nataka unitoroshe tuishi pamoja kama mume na mkewe. Sitaki uzee tena, natamani ujana wakati ninapoweza kuufaidi. Tafadhali nisaidie, hutajuta. 

                                                Akupendaye kufa na kuzikana

Mama Furaha 

                                    Wakati anapoisoma barua, Mzee Mkali, kila baada ya sentensi mbili tatu, anaacha kusoma na kumtupia Mama Furaha jicho la chuki. Mama Furaha naye anaonyesha kushikwa na kimbimbi na kutaka kutoroka. 

Mzee Mkali:              Haya, Mama Furaha, maneno yako yameniingia sawasawa. Kuanzia saa hii wewe sio mke wangu tena na ninakutaka uondoke hapa katika nyumba hii sasa hivi kabla giza halijaingia. Vikorokoro vyako utavikuta huko huko kwenu. Ondoka hapa! 

                                    Mama Furaha anapiga magoti mawili huku anainamisha kichwa kwa soni na kulia machozi hali anasema “mume wangu, mume wangu, mume wangu.” Mzee anaondoka polepole na Sitaki na Bi Saada nao pia wanaondoka wakimwacha Mama Furaha peke yake katika hali ya unyonge na jitimai.

Sitaki na mchumbake Saada waanza kuondoka jukwaani wakishikana mikono mithili ya vijana wapendanao. Ghafla Bi Saada anaacha kuushika mkono wa Sitaki huku akielekeza kidole kwa mchumbake na kusikika kutamka “Jihadhari mpenzi, dunia hii ina mambo, wako wezi wa kila aina.” Sitaki naye anainamisha kichwa chake kwa aibu na huzuni.  
10/10/04



Reference
362
Grammar
Vocabulary

Special Characters
Instructors Notes


© 2002 Rutgers University, excluding excerpted material that remains under the ownership of the existing copyright holders.

digiclass_help@brokenmail.rutgers.edu please replace "brokenmail" with ctaar.rutgers.edu