Nafanya kazi ofisini. Mchumba wangu
ana-taka niache kazi nikae nyumbani. Ameahidi kunipa kila mwezi mara
mbili ya mshahara wangu wa sasa. Nampenda kufa, na ningetaka
niolewe1 naye. Nifanye nini?
Ijapokuwa unampenda
kufa lakini huna budi2 umwulize au ujiulize mwenyewe maswali
machache. Je, ni kwa nini hataki uendelee kufanya kazi? Je, anatazamia kukuoa
lini? Je, uchumba wenu ukivunjika itakuwaje?3
Je, akifungwa, au
akiugua, au donge analopata likitoweka wewe utakuwa wapi? Je,
maisha ya kuzurura nyumbani bila kazi ni kitendo cha
maendeleo?
Ni dhahiri kuna kitu huyu mchumba
anacho-kiogopa ikiwa4 utazidi kuendelea5 na kazi yako huko ofisini. Pengine ana
wivu6 kwamba huko ofisini una wapenzi wengine.
Pengine anahofia kwamba utakutana na7 wengine huko ambao
watakunyakua. Kwa vyovyote8 huyu mchumba hafikirii
maslahi yako bali yake mwenyewe. Ikiwa ameanza kukufuga na
kukupa masharti hivi mapema kwenyeuchumba, je akishakuoa
unatazamia uhuru wa aina gani? Maoni yetu ni kwamba mchumba huyu
hakufai. Achana9 naye.
Niko masomoni bado, mchumba
wangu ambaye nampenda
sana anataka tuoane mapema. Je, niache masomo au
nimwache yeye?
Kama upo uwezekano10 wa kuendelea na masomo yako baada ya
kuoana hakuna sababu yo yote ya kumwacha. Vilevile kama unao uhakika
kwamba maisha yenu katika ndoa yatakuwa mazuri ni afadhali usikubali
kumpoteza. Lakini si vizuri ukatishe masomo yako kwa
kumkimbilia mchumba ambaye huna hakika ya maisha yako naye baadaye. Kwa
kuwa masomo yako yatakuwa na faida11 kwenu wawili na pia kwa jamaa na
nchi nzima, itafaa12 umtafadhalishe mchumba wako
akusubiri mpaka umalize masomo.
Ikiwa kweli naye anakupenda bila shaka atakubali. Akikataa, na ukiona
kwamba hana sababu kubwa ya kutaka
mwoane mapema, basi unaweza kukataa kukatisha masomo yako. Hapo
itakuwa hiari yake kukungojea ama kutafuta mchumba
mwingine. Mara nyingi wachumba wanaotaka kuvunjia wenzao13 masomo huwa ni14 wale wenye wasiwasi kwamba
huenda wakapigwa teke15 hapo baadaye.
1. Mwandishi wa kwanza ni mwanamke au mwanamume? Unajuaje?
2. Kama mwandishi wa kwanza akikubali kukaa
nyumbani, mchumba wake amesema kwamba
atafanyaje?
3. Waandishi wa barua hizi ni wafanya kazi au sivyo?
4. Mwandishi wa pili ana shida gani?
5. Je,
Majibu katika somo ni kama yale ambayo wazazi au ndugu
wangetoa? Au ni kama majibu ya watu ambao hawajakutana na
wanaouliza? Unajuaje?
6. Eleza kwa ufupi namna za woga ambazo wachumba wengine
wanazo.
7.
Maandishi kama hayo kwa kawaida hupatikana wapi? Toa mfano mmoja wa maandishi
mengine ya aina hii.
8. Anayejibu anasema ni afadhali mwandishi wa pili afanyeje?
9. Rafiki
yako akikuuliza maswali kama yaliyomo katika somo,
utajibuje? Eleza kwa ufupi.
-----------------------------------------------------------------
MSAMIATI
mchumba/wachumba - kijana aliyeposa au aliyeposwa
kuahidi - mtu kusema kwamba bila shaka atafanya kitu fulani
kupenda kufa - kupenda
sana
anatazamia kukuoa lini - anafikiri kukuoa lini
uchumba - hali ya kuwa na mpango wa kuoana
kufungwa - kukamatwa na polisi na kuwekwa mahali mbali ya
wengine kwa sababu ya kukosa
kuugua - kupata ugonjwa
donge analopata likitoweka - kama hatakuwa
na mshahara
kuzurura nyumbani - kuweko nyumbani tu, bila kitu cha maana cha
kufanya
kitendo cha maendeleo/vitendo vya maendeleo - jambo
linalofanya maisha yawe bora
ni dhahiri - ni rahisi kuona au kufahamu
kuogopa - kuwa na woga
kuwa na wivu - kufikiri pengine mpenzi wako ana wapenzi
wengine
kuhofia - kuogopa
kukutana na - kuonana na mtu fulani kwa mara ya kwanza
kunyakua - kuchukua
maslahi – faida
uwezekano – njia ya kuweza, hali ya kuwezekana
uhakika – hali ya kutokuwa na shaka
kupoteza – kukosa kukiona (kitu)
kukatisha masomo yako – kuacha kusoma
kukimbilia – kumfuata mtu bila kutumia akili
kutafadhalisha – kusema “tafadhali”
kusubiri – kungoja
kufuga - kuweka, mtu, mnyama au ndege nyumbani ili
asitoke
kupa masharti – kulazimisha kufanya kitu
maoni – mawazo
kufaa – kuwa na faida
kuachana na – kutoendelea na (mpenzi)
hiari – kuchagua
kuvunja - kufanya kitu kivunjike